Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Habari la Hawza, Makao Makuu ya Haki za Binadamu katika taarifa yake imelaani hatua ya hivi karibuni ya serikali ya Imarati ya kufuta leseni za shughuli za shule za Kiirani na kuwafukuza wanafunzi kwa utaratibu maalumu kutoka katika mazingira ya elimu, na ikatangaza: Mwenendo huu ambao umefanyika chini ya kivuli cha mvutano wa kisiasa na kwa misukumo ya kiuadui, si hatua rahisi ya kiutawala tu, bali ni mfano wazi wa ukiukwaji wa kimfumo wa wajibu wa kimataifa wa serikali ya Imarati chini ya mikataba ya haki za binadamu, hususan Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni (ICESCR).
Matini ya taarifa hiyo ni kama ifuatavyo:
Hatua ya hivi karibuni ya serikali ya Imarati ya kufuta leseni za shughuli za shule za Kiirani na kuwafukuza wanafunzi kwa utaratibu maalumu kutoka katika mazingira ya elimu ni jambo ovu na linalopingana na misingi iliyo wazi ya sheria za kimataifa. Mwenendo huu ambao umefanyika chini ya kivuli cha mvutano wa kisiasa na kwa misukumo ya kiuadui, si hatua rahisi ya kiutawala tu, bali ni mfano wazi wa ukiukwaji wa kimfumo wa wajibu wa kimataifa wa serikali ya Imarati chini ya mikataba ya haki za binadamu, hususan Mkataba wa Haki za Mtoto (CRC) na Mkataba wa Kimataifa wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kitamaduni (ICESCR). Inasikitisha sana kwamba serikali ambayo hujiita “Aal Sabri wa Tasamuh” imekanyaga misingi ya uvumilivu kwa kundi lisilo na ulinzi zaidi miongoni mwa wanadamu, yaani watoto wasio na hatia, na imebadilisha usalama wa kielimu kwa njaa ya kielimu na msukosuko wa kisaikolojia.
Kwa mtazamo wa sheria za kimataifa, kile kilichotokea huko Imarati kinapingana moja kwa moja na kanuni ya msingi ya “kupiga marufuku adhabu ya pamoja”. Makao hii makuu inaamini kwa nguvu zote kwamba; kufutwa kwa leseni za shughuli za shule za Kiirani si chochote isipokuwa ni shinikizo la kisiasa kupitia kuufanya mustakabali wa kielimu wa maelfu ya watoto wasio na hatia kuwa mateka. Jambo hili linapingana kikamilifu na kifungu cha kwanza cha ibara ya 28 ya Mkataba wa Haki za Mtoto, ambayo huzilazimisha serikali wanachama kuchukua hatua zote muhimu za kuhakikisha upatikanaji sawa wa elimu, ikiwemo elimu ya msingi ya lazima na ya bure kwa wote.
Serikali ya Imarati kwa hatua hii imekiuka mfumo maalumu wa kanuni ya kutobagua ambayo imejidhihirisha katika ibara ya 2 ya Mkataba wa Haki za Mtoto. Roho ya ibara hii ni kupiga marufuku kabisa aina yoyote ya ubaguzi, kunyimwa haki au kuwekwa mipaka kwa msingi wa utaifa katika kufaidika na haki za watoto. Kufunga milango ya shule kwa watoto wa taifa maalumu si dosari ya kiufundi, bali ni ubaguzi uliopangwa kwa msingi wa uraia na utaifa ambao unapingana kabisa na falsafa ya kuwepo kwa Mkataba wa Umoja wa Mataifa na heshima ya asili ya mwanadamu. Mwenendo huu wa kibaguzi pia uko wazi kuwa unapingana na kifungu cha pili cha ibara ya 2 ya Mkataba wa Haki za Mtoto, ambayo huzilazimisha serikali kuwalinda watoto dhidi ya aina yoyote ya ubaguzi; wajibu ambao Imarati katika tukio hili imefanya kinyume chake kabisa na yenyewe ikageuka kuwa chanzo cha ubaguzi.
Katika uchambuzi wa kina zaidi wa kisheria, ukiukwaji wa wajibu wa “kuzingatia maslahi ya juu ya mtoto” (ibara ya 3 ya Mkataba wa Haki za Mtoto) unaonekana wazi kabisa. Kwa mujibu wa mkataba huo na maoni ya jumla ya Kamati ya Haki za Mtoto, kila hatua ya kiutawala na kisheria inayowaathiri watoto lazima kabla ya utekelezaji wake ipitie tathmini ya athari kwa mtoto.
Maoni yako